Ijumaa, 7 Februari 2014

Mvua iliyoambatana na upepo mkali uliovuma usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam umesababisha umeme kukatika kwa zaidi ya saa sita katika sehemu kubwa ya jiji hilo,miti kuanguka pamoja na wavuvi kusitisha shughuli za uvuvi ili kunusuru maisha yao huku mamlaka ya hali ya hewa ikisema upepo kama huo huenda ukaendelea kutokea nchini hadi Jumatano ijayo.

Swahili vibe imepita katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es salaam majira ya asubuhi na kushuhudia miti ikiwa imeanguka pembezoni  mwa barabara pamoja na nguzo za umeme zikiwa katika hali ya kutaka kudondoka .
Katika sehemu kubwa ya jiji la Dar es Salaam umeme ulikatika wakati upepo huo ukivuma  ambapo  mafundi wa  shirika la umeme Tanzania -Tanesco wameonekana  majira hayo ya asubuhi wakiwa katika harakati za kurejesha umeme.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni