Napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa fursa
ya kuiona siku nyingine nikiwa na Afya njema
kabisa,Mapema leo mchana,ilikuwa ni
siku niliyopanga kutimiza ahadi
yangu ya Kuwapeleka shule watoto
walioshinda shindano la kucheza ngololo..
na kwa vile nilitaka wapate elimu iliyo bora
zaidi,nilikaa na management yangu..na
kutafiti ni shule ipi itakayokidhi mahitaji ya watoto wale,shule yenye
mazingira mazuri
ya kusomea
na yenye standard nzuri.
sote tulikubaliana kuwapeleka shule ya
EAST AFRICA INTERNATION SCHOOL,iliyopo Mikocheni.
napenda kumshukuru mkuu wa shule hii,Bi Mercy
Githirua kwa kutupokea vizuri mimi na
watoto wale..lakini pia kuwashukuru wanafunzi wote kwa kutupokea vizuri
Nikisarimiana na mkuu wa shule bi,Mercy Githirua
Nilipata nafasi ya kuzungmza na
wanafunzi na kuwausia mambo
mbalimbali ya kimaisha....
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni